KLABU ya Arsenal jana ilipunguzwa kasi yake katika
Ligi Kuu ya England baada ya kulazimishwa sare ya bao 1-1 na Everton katika
mchezo uliochezwa kwenye uwanja wa nyumbani wa Emirates jijini London.
Arsenal ndiyo walikuwa wa kwanza kupata bao la
kuongoza kupitia kwa kiungo Mesut Ozil dakika ya 80, lakini Gerard Deulofeu
aliyetokea benchi akaisawazishia Everton dakika ya 84 na kufanya timu hizo
kugawana pointi katika mchezo huo.
Everton hata hivyo hawakuwa na wasiwasi wa mchezaji
yeyote kuwa na jeraha. Antolin Alcaraz alikuwa kwenye kikosi hicho lakini
Leighton Baines, Arouna Kone na Darron Gibson walisalia nje.
Licha ya kuongoza orodha kwa pointi tano sasa,
baadhi wana shauku ikiwa kweli Arsenal inaweza kushinda kombe hilo msimu huu kwa
sababu ushawishi wao kuweza kufanya hivyo bado haujawagusa mashabiki wengi wa
soka.
0 comments