Open top menu
Jumatatu, 9 Desemba 2013

KLABU ya Arsenal jana ilipunguzwa kasi yake katika Ligi Kuu ya England baada ya kulazimishwa sare ya bao 1-1 na Everton katika mchezo uliochezwa kwenye uwanja wa nyumbani wa Emirates jijini London.

Arsenal ndiyo walikuwa wa kwanza kupata bao la kuongoza kupitia kwa kiungo Mesut Ozil dakika ya 80, lakini Gerard Deulofeu aliyetokea benchi akaisawazishia Everton dakika ya 84 na kufanya timu hizo kugawana pointi katika mchezo huo. 

Everton hata hivyo hawakuwa na wasiwasi wa mchezaji yeyote kuwa na jeraha. Antolin Alcaraz alikuwa kwenye kikosi hicho lakini Leighton Baines, Arouna Kone na Darron Gibson walisalia nje.


Licha ya kuongoza orodha kwa pointi tano sasa, baadhi wana shauku ikiwa kweli Arsenal inaweza kushinda kombe hilo msimu huu kwa sababu ushawishi wao kuweza kufanya hivyo bado haujawagusa mashabiki wengi wa soka.

Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments