Open top menu
Jumatatu, 23 Septemba 2013


MSANII nyota wa filamu na muziki, Snura Mushi 'Snura' amevunja ukimya na kuwaambia wanaume wakware kuwa hatumii kiuno chake kutafuta mabwana bali anakitumia kusaka pesa.

Snura amelazimika kufungua kwa style hiyo kutokana na usumbufu anaoupata kutoka kwa wanaume ambao wanapagawa na jinsi anavyomudu kuzungusha kiuno jukwaani kwani pamoja na kudata lakini hawataweza kukiona 'live'.

Msanii huyo anayetamba na nyimbo zake za Majanga na Nimevurugwa, aliiambia Nyumba ya Michezo na Burudani kuwa kuna wanaume wengi wanadhani anapokatika viuno kwenye show zake basi anatafuta wanaume huku wakisahau kuwa ile ni kazi inayompa kula.

Alisema inawezekana wanaume wakawa wanakitamani na wanaamini kuwa anakitumia kwa ajili ya mapenzi na kuwadatisha wenye hela, ingawa ndani ya nafsi yake anajua nini anachokifanya na hayuko kama mastaa wengine wanaishi mjini kwa nguvu za wanaume.

"Mimi sipo kama mastaa wengine, natumia kiuno changu kusaka pesa  na si wanaume,” alisema Snura. “Kiuno change ndicho kinanipa kula na ndiyo maana kila siku manjonjo yanaongezeka.”
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments