MSHIRIKI aitwaye Hope toka Burundi amejikuta
akianguka chini kwa mshituko wa furaha ulimkuta baada ya kuibuka kidedea kwa
kutangazwa mshindi wa Tusker Project Fame na kujinyakulia kitita cha Shilingi
5,000,000/= za Kenya.
Mashindano hayo yaliyomalizika hivi punde usiku huu
yamemwacha Hope katika taharuki huku akiwabwaga washiriki wenzake, Hisia
(Tanzania), Patrick (Rwanda), Wambura (Kenya), Daisy (Uganda), Amos & Josh
wa Kenya
Sauti ya pekee ya kijana huyo imeibua thamani yake
katika tasnia ya muziki, Hope hakuwahi kufanya video ya wimbo wowote zaidi ya
ule uliompatia ushindi wa Tusker.
0 comments