Open top menu
Jumanne, 10 Desemba 2013

FIFA imethibitisha orodha ya majina ya wachezaji watatu walioingia fainali ya kuwania tuzo ya Mwanasoka Bora wa Dunia wa mwaka 2013, Ballon d'Or ambao ni mtetezi Lionel Messi, Cristiano Ronaldo na Franck Ribery.

Messi ameshinda mfululizo mara nne tuzo zilizopita, lakini safari hii ni Ronaldo anayepewa nafasi kubwa ya kutwaa mpira wa dhahabu.

Mshindi mtarajiwa, Messi anaweza kupokonywa tuzo hiyo na Ronaldo kutokana na mchezaji huyo Real Madrid kuwa juu hivi sasa

Mshambuliaji huyo wa Real Madrid, amefunga mabao 32 tayari msimu huu kwa klabu na timu yake ya taifa, huku Messi kwa sasa yupo nje ya kikosi cha Barcelona kutokana na maumivu ya nyama.

Mabao yake matatu aliyofunga peke yake, hat-trick wakati Ureno inaifunga 3-2 Sweden katika mechi maalum ya kufuzu Kombe la Dunia, yameongeza hamasa za watu kumpendekeza kutwaa tuzo hiyo kwa mara ya pili katika historia yake.

Ribery, aliyeiwezesha Bayern Munich kutwaa taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya, alikuwa anapewa nafasi kubwa ya kuishinda kabla ya Ronaldo kufanya mambo makubwa dhidi ya Sweden na FIFA ikaongeza muda wa kupigia kura washindani.

Mshindi atatangazwa katika usiku wa hafla maalum ya Ballon d'Or mjini Zurich, Uswis Januari 13, mwakani.

Wakati huo huo, FIFA pia imethibitisha orodha ya wachezaji wanaowania kuwamo katika kikosi cha wachezaji 11 bora wa dunia, FIFPro World XI 2013.

Kuna wachezaji wanne wa England kwenye orodha hiyo ambao ni Leighton Baines, Ashley Cole, Steven Gerrard na Wayne Rooney.

Wachezaji ambao wanatarajiwa kushindania kuingia katika kikosi hicho ni:-
Makipa:
Gianluigi Buffon (Italy, Juventus); Iker Casillas (Spain, Real Madrid CF); Petr Cech (Czech Republic, Chelsea FC); Manuel Neuer (Germany, FC Bayern München), Víctor Valdes (Spain, FC Barcelona).

Mabeki:
David Alaba (Austria, FC Bayern München); Jordi Alba (Spain, FC Barcelona); Dani Alves (Brazil, FC Barcelona); Leighton Baines (England, Everton FC); Jérôme Boateng (Germany, FC Bayern München);Ashley Cole (England, Chelsea FC); Dante (Brazil, FC Bayern München); Mats Hummels (Germany, Borussia Dortmund); Branislav Ivanović (Serbia, Chelsea FC); Vincent Kompany (Belgium, Manchester City FC); Philipp Lahm (Germany, FC Bayern München); David Luiz (Brazil, Chelsea FC); Marcelo (Brazil, Real Madrid CF); Pepe (Portugal, Real Madrid CF); Gerard Piqué (Spain, FC Barcelona); Sergio Ramos(Spain, Real Madrid CF ); Thiago Silva (Brazil, Paris St-Germain FC); Raphaël Varane (France, Real Madrid CF); Nemanja Vidić (Serbia, Manchester United FC); Pablo Zabaleta (Argentina, Manchester City FC).

Viungo:
Xabi Alonso (Spain, Real Madrid CF); Gareth Bale (Wales, Tottenham Hotspur FC/Real Madrid CF);Sergio Busquets (Spain, FC Barcelona); Steven Gerrard (England, Liverpool FC); Andrés Iniesta (Spain, FC Barcelona); Isco (Spain, Málaga CF/ Real Madrid CF); Mesut Özil (Germany, Real Madrid CF/Arsenal FC); Andrea Pirlo (Italy, Juventus); Marco Reus (Germany, Borussia Dortmund); Franck Ribéry (France, FC Bayern München), Arjen Robben (Netherlands, FC Bayern München); Bastian Schweinsteiger(Germany, FC Bayern München); Yaya Touré (Côte d’Ivoire, Manchester City FC); Arturo Vidal (Chile, Juventus); Xavi  (Spain; FC Barcelona).

Washambuliaji:

Sergio Agüero (Argentina, Manchester City FC); Mario Balotelli (Italy, Manchester City FC/AC Milan); Edinson Cavani (Uruguay, SSC Napoli/Paris Saint-Germain FC); Diego Costa (Spain, Club Atlético de Madrid); Cristiano Ronaldo (Portugal, Real Madrid CF); Didier Drogba (Côte d’Ivoire, Shanghai Shenhua FC/Galatasaray SK); Radamel Falcao (Colombia, Club Atlético de Madrid/AS Monaco FC); Zlatan Ibrahimovi (Sweden, Paris Saint-Germain FC); Robert Lewandowski (Poland, Borussia Dortmund); Mario Mandžukić (Croatia, FC Bayern München); Lionel Messi (Argentina, FC Barcelona); Neymar (Brazil, Santos FC/FC Barcelona); Wayne Rooney (England, Manchester United FC); Luis Suárez (Uruguay, Liverpool FC); Robin van Persie (Netherlands, Manchester United FC).
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments