Open top menu
Alhamisi, 12 Desemba 2013

KLABU ya Barcelona jana iliingia hatua ya 16 Bora kwa kishindo baada ya kuitandika Celtics mabao 6-1 huku mshambuliaji wake wa  Brazil, Neymar akipiga hat-trick yake ya kwanza barani Ulaya.

Licha ya Barcelona kuwakosa Andres Iniesta aliyebaki benchi, Leonel Messi ambaye bado majeruhi na Cesc Fabregas anayetumikia adhabu, imeendeleza makali yake ya kutoa kichapo hicho cha mbwa mwizi.

Neymar aliyeongoza safu ya ushambuliaji hakufanya makosa baada ya kufunga hat trick yake ya kwanza katika Ligi ya Mabingwa dakika za 45, 48 na 58, wakati mabao mengine yalifungwa na Pique dakika ya saba, Pedro dakika ya 39, na Tello dakika ya 72. 

Kwa upande wa Arsenal wao wameponea chupuchupu kukosa hatua ya 16 bora baada ya kukubali kipigo cha mabao 2-0 kutoka kwa Napoli ya Italia na kufanya timu zote tatu za kundi F zikifungana kwa pointi baada ya kumaliza wakiwa na pointi 12 na mabao ndiyo yaliyoipeleka hatua ya mtoano.

Arsenal ambayo walimaliza mchezo huyo wakiwa pungufu baada ya dakika ya 76, nahodha wake, Mikel Arteta alipotolewa nje kwa kadi nyekundu hali iliyosababisha kuleta udhaifu katika kikosi cha Arsene Wenger. 

Mabao ya Napoli yamefungwa na Gonzalo Higuain dakika ya 73 Callejon dakika ya 90.

Katika mchezo mwingine, timu ya Chelsea ilifanikiwa kuibuka na ushindi wa bao 1-0 bao pekee lilofungwa na Demba Ba dakika ya 11, limempa faraja kocha Jose Mourinho wa Chelsea kwa ushindi huo dhidi ya Steaua Bucharest.

Mapema mchana wa jana katika mchezo wa kiporo, bao pekee la Wesley Sneijder liliipa ushindi wa 1-0 nyumbani Galatasaray dhidi ya Juventus na kufuzu 16 Bora, huku Kibibi Kizee cha Turin kikifungishwa virago. 


Katika mechi nyingine za usiku huu, Marseille imefungwa 2-1 nyumbani na Borussia Dortmund, Atletico de Madrid imeidunga 2 - 0 FC Porto, FC Schalke 04 imeifunga 2 - 0 Basel, FK Austria Wien imeifunga 4-1 Zenit St Petersburg, AC Milan imetoka sare ya  0-0 na Ajax.

Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments