Open top menu
Jumapili, 8 Desemba 2013

BONANZA la mchezo wa mpira wa miguu litakaloshirikisha timu mbalimbali za Veterani za mkoani Morogoro linatarajiwa kufanyika Desemba 14 na 15, mwaka huu, katika uwanja wa Shujaa, mjini hapa.

Akizungumza na mtandao huu, mratibu wa bonanza hilo, Daudi Julian alisema lengo la bonanza hilo, ni kuwakutanisha pamoja wanasoka wa zamani na kuimarisha afya zao.

Julian alisema maandalizi kuendelea bonanza hilo linalosubiriwa kwa hamu kubwa yanakwenda vizuri huku timu shiriki zikiwa katika mazoezi makali.

Mratibu huyo alizitaja baadhi ya timu zinazotarajia kushiriki katika bonanza hilo kuwa ni Moro Veterani, Reli Family Veterani, Kihonda Veterani, Mzumbe Veterani, Kichangani Veterani, Burkina Faso Veterani, Mazimbu Veterani na Shooting Stars Veterani.

“Maandalizi yanakwenda vizuri na tayari baadhi ya timu zimethibitisha kushiriki,” alisema.

Aidha, Julian alisema zawadi mbalimbali zinatarajiwa kutolewa kwa timu zitakazofanya vizuri ikiwemo pia zawadi kwa mchezaji mmoja mmoja.


“Hili bonanza ni la aina yake na kwamba halijawahi kufanyika mkoani Morogoro na niseme huu ni mwanzo tu, mabonanza zaidi yanakuja,” alisema.
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments