BONANZA la mchezo wa mpira wa miguu
litakaloshirikisha timu mbalimbali za Veterani za mkoani Morogoro linatarajiwa
kufanyika Desemba 14 na 15, mwaka huu, katika uwanja wa Shujaa, mjini hapa.
Akizungumza na mtandao huu, mratibu wa bonanza hilo,
Daudi Julian alisema lengo la bonanza hilo, ni kuwakutanisha pamoja wanasoka wa
zamani na kuimarisha afya zao.
Julian alisema maandalizi kuendelea bonanza hilo
linalosubiriwa kwa hamu kubwa yanakwenda vizuri huku timu shiriki zikiwa katika
mazoezi makali.
Mratibu huyo alizitaja baadhi ya timu zinazotarajia
kushiriki katika bonanza hilo kuwa ni Moro Veterani, Reli Family Veterani,
Kihonda Veterani, Mzumbe Veterani, Kichangani Veterani, Burkina Faso Veterani,
Mazimbu Veterani na Shooting Stars Veterani.
“Maandalizi yanakwenda vizuri na tayari baadhi ya
timu zimethibitisha kushiriki,” alisema.
Aidha, Julian alisema zawadi mbalimbali zinatarajiwa
kutolewa kwa timu zitakazofanya vizuri ikiwemo pia zawadi kwa mchezaji mmoja
mmoja.
“Hili bonanza ni la aina yake na kwamba halijawahi
kufanyika mkoani Morogoro na niseme huu ni mwanzo tu, mabonanza zaidi yanakuja,”
alisema.
0 comments