VINARA wa Ligi Kuu ya England, Arsenal wamerudi
katika nafasi yao baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Cardiff
City uliochezwa kwenye Uwanja wa Emirates.
Arsenal imeipiga kikumbo Manchester City ambao
walikaa kileleni kwa saa moja baada ya kufikisha pointi 45 na kuwaacha City
wakiwa na pointi 44.
Washika Bunduki hao wa London ilibidi wasubiri hadi
dakika ya 88 baada ya mshambuliaji wake, Nicklas Bendtner kuwamisha mpira
wavuni lakini dakika mbili baadaye Theo Walcott aliongeza bao la pili.
Katika mchezo mwingine uliochezwa leo, Liverpool nao
wamefanikiwa kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Hull City na kuwafanya
kuchuka hadi nafasi ya nne kutoka nafasi ya tano, baada ya kufikisha pointi 39.
Mabao ya
Liverpool yamefungwa na Daniel Agger dakika ya 36 wakati bao la pili liliwekwa
kimiani na Luis Suarez dakika ya 50 ya mchezo huo.
Mabao ya Fernando Torres, Willian na Oscar
yaliiwezesha timu ya Chelsea kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya
Southamptom katika mchezo uliochezwa mapema leo.
Matokeo ya michezo mingine iliyochezwa mapema leo,
Crystal Palace walitoshana nguvu na Norwich City baada ya kutoka sare ya mabao
1-1, Fulham leo imezinduka na kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya West Ham
United na Stoke City wamegawana pointi ya Everton kwa kutoka sare ya mabao 1-1, West Brom wameibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Newcastle United.
0 comments