TIMU ya Manchester City imefanikiwa kuishusha
kileleni Arsenal baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Swansea katika
mchezo mgumu uliomalizika muda mfupi uliopita.
Man City imekaa kileleni baada ya kujikusanyia
pointi 44 na kuiacha kwa pointi mbili Arsenal ambao walimaliza mwaka uliopita
wakiwa kileleni kwa pointi 42.
Lakini Man City inaweza kusherehekea nafasi hiyo kwa
muda mfupi kama Arsenal watashinda mchezo wao dhidi ya Cardiff City unaochezwa
kwenye Uwanja wa Emirates.
Mabao ya Man City yalifungwa na Fernandinho dakika
ya 14, Yaya Toure dakika ya 58 na Aleksandar kolarov dakika ya 66 wakati mabao
ya Wilfried Bony dakika ya 45 na 90.
0 comments