MWANAMUZIKI wa Hip Hop nchini, Fareed Kubanda ‘Fid Q’
amewagomea Madj wa Clouds na kuacha kuimba na kushusha jukwaani baada ya madj
kushindwa kumpigia ala za muziki ‘beat’ na badala yake kupiga wimbo kamili.
Fid Q alionyesha ukomavu leo katika tamasha ya
kusherehekea miaka 14 ya kituo cha redio cha Clouds baada ya kumwambia Dj Zero
kupiga beat ya wimbo wake lakini dja huyo hakufanya hivyo na badala yake
akaweka mic chini ya kushuka jukwaani.
Wasanii wote waliopanda katika tamasha hilo lililoandaliwa
na Clouds redio walikuwa wakiimba nyimboa zao kamili kwa kurudia maneno yao
yaliyorekodiwa kitu ambacho kilikuwa tofauti kwa Fid Q.
0 comments