KLABU ya Chelsea inaweza kuharibu mipango ya
Liverpool ya kumsajili winga wa FC Basel, Mohamed Salah baada ya kuweka mezani
dau ya pauni 11 milioni ambazo ni zaidi ya kiasi kilichotengwa na Majogoo wa
Anfield.
FC Basel walikuwa tayari kumuuza nyota huyo wenye
umri wa miaka 21, kwa dau la pauni 10 milioni lakini Liverpool walikuwa tayari
kutoa pauni 7 milioni.
Jose Mourinho amevutiwa na mchezaji huyo ambaye
aliwafunga katika michezo yote miwili waliokutana katika michuano ya Ligi ya
Mabingwa Ulaya hatua ya makundi.
Pamoja na Salah kunukuliwa aakisema kuwa atafurahi
zaidi kisaini kuichezea Liverpool lakini dau kubwa la Chelsea linaweza kuharibu
mipango hiyo.
0 comments