Open top menu
Alhamisi, 23 Januari 2014

UFAMLE wa klabu ya Manchester United umezidi kuporomoka baada ya kupokwa nafasi ya kwanza kuwa klabu tajiri duniani na nafasi hiyo sasa inashikiriwa na Real Madrid ya Hispania.

Manchester United ambayo sasa ipo katika msimu mbaya baada ya kupoteza matumaini ya kutetea ubingwa wake wa Ligi Kuu ya England lakini sasa imepoteza heshima ya nje ya uwanja.

Klabu hiyo ambayo ilikuwa nafasi ya kwanza mwaka jana lakini sasa imetupwa mpaka nafasi ya nne, kwani nafasi tatu za juu zimechukuliwa na Madrid, Barcelona ya Hispania na Bayern Munich ya Ujerumani.

Madrid imeshika nafasi hiyo baada ya kuingia zaidi ya euro 518 milioni katika msimu wa 2012/13, wakifuatiwa na Barcelona iliyoingia euro 482 milioni wakati Bayern inashika nafasi ya tatu ikiingiza euro 431.

Nafasi ya nne ipo Manchester United iliyoingia euro 423 na Paris Saint-Germain ‘PSG’ ya Ufaransa imeshika nafasi ya tano kwa kuingiza euro 398 milioni.


Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments