Open top menu
Jumanne, 17 Septemba 2013


NAHODHA wa timu ya Manchester City, Vincent Kompany anatarajia kurudi uwanjani leo katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Viktoria Plzen baada ya kuwa majeruhi toa kuanza kwa msimu huu.

Beki huyo wa kati mwenye umri wa miaka 27, alikuwa nje ya uwanja baada ya kuumia nyonga katika mchezo wa kwanza wa ufunguzi wa Ligi Kuu ya England na timu yake imeshinda mchezo mmoja kati ya mitatu waliyocheza bila nyota huyo.

Kocha Mkuu wa Manchester City, Manuel Pellegrini amesema kuwa nyota huyo wa Ubelgiji kwa sasa yupo fiti japokuwa hakucheza katika mchezo wa timu yake ya taifa dhidi ya Jamhuri ya Czech.

"Vincent amefanya mazpoezi na sisi kwa siku mbili zilizopita," alisema Pellegrini. "Tutaangalia kama atakuwa fiti kwa asilimia 100. Kama atakuwa fiti atacheza leo. Tutazungumza na daktari wa timu na kutoa maamuzi.

"Nadhani yupo fiti kwa asilimia 100, lakini kama itakuwa toifauti hatutamtumia. Tunakabiliwa na mchezo mgumu na muhimu sana kweli lakini tutawatumia wachezaji wengine kama yeye hatakuwa fiti."
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments