Open top menu
Jumatatu, 9 Septemba 2013


MCHEZA tenisi namba moja kwa ubora duniani kwa wanawake, Serena Williams jana alishinda taji lake la tano ya mashindano ya US Open baada ya kumgalagalaza Victoria Azarenka katioka fainali ya mchjezo huo uliochezwa kwenye Uwanja wa Flushing Meadows.

Mwanadada huyo wa Kimarekani mwenye umri wa miaka 31, alishinda mchezo huo kwa 7-5 6-7 (6-8) 6-1 ikiwa ni mara ya pili kukutana na mchezaji huyo wa Belarusia.

Taji hilo ni la 17 kwa Serena ambaye sasa amefikia rekodi ya Martina Navratilova na Chris Evert, hivyo kubakisha mataji saba kumfikia anayeshikilia rekodi ya kuwa na mataji 24 iunayoshikiliwa na Margaret Court's.

"Nilikutana na ushindani mkubwa sana, ni mpiganaji mkubwa sana na hiyo ndiyo maana alistahili kushinda mataji makubwa mawili," anasema Serema alipokuwa anamzungumzia Azarenka baada ya mchezo kumalizika.
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments