Open top menu
Jumatano, 4 Septemba 2013


Hali ndani ya klabu ya Yanga ni tete, baada ya wazee wa Yanga kutokubali maamuzi yaliyofanya na uongozi wa juu wa klabu hiyo chini ya Mwenyekiti wake, Yussuf Manji.

 Wazee hao wakiongozwa na Mzee Ibrahim Ally Akilimali waliiambia Nyumba ya Michezo na Burudani kuwa hawakubaliani na kitendo cha uongozi wa Yanga kumuajiri Katibu Mkuu kutoka Kenya pamoja na Mhasibu mwenye asili ya Kiasia.

Wazee hao walisema wamesikia kuwa Manji amemleta katibu kutoka Kenya anaitwa Patrick Naggi anayechukua nafasi ya Lawrence Mwalusako aliyemaliza Mkataba wake na Mhasibu Mhindi, kitu ambacho hawakubaliani nacho.

Wazee hao ambao ndiyo walioilaani klabu hiyo wakati wa uongozi wa Lloyd Nchunga na kusababisha timu hiyo kuchapwa mabao 5-0 na Simba katika mchezo wao wa mwisho katika misimu miwili iliyopita.

Kama mgogoro huo ukiendelea kuna uwezekano laana hiyo ikarudi tena kwa klabu hiyo kwani wakati vuguvugu hilo likianza kufukuta ni mwezi mmoja na siku kadhaa kabla ya kuchezwa mchezo wa watani wa jadi uliopangwa kufanyika Oktoba 20, mwaka huu kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. 
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments