Open top menu
Jumanne, 24 Septemba 2013


 MREMBO anayetikisa kwenye tasnia ya filamu Bongo, Skyner Ally Seif anayependa ukimwita 'Skyner', amewapasha wasanii wenzake wasijidanganye na majina waliyokuwa kuwa nayo kwenye movie na kuamini kuwa wanaweza kufanya vizuri kwenye siasa.

Skyner ambaye anafanya vizuri katika tasnia hiyo kwa sasa amesema kuwa kwa upande wake hafikirii kujiingiza kwenye siasa kama wanavyofanya wasanii wengine wa filamu na muziki kwa sasa kwani anaamini kuwa mambo hayo siyo rahisi kama wengine wanavyofikiria.
Msanii huyo aliiambia Nyumba ya Michezo na Burudani kuwa wasanii wengi wanaingia kwenye siasa wakiamini kuwa kuna fedha nyingi na wanasahau kuwa siasa inahitaji kuwa na moyo wa kujitolea na kuwatumikia wananchi kitu ambacho anaamini wasanii wengi hawana moyo huo.

Alisema kuna kazi nyingi za kufanya na siyo siasa pekee, hivyo anaamini kwa upande wake sanaa ni changua lake kubwa ambalo linaweza kuinua maisha yake na kumpeleka mbali zaidi.

"Binafsi sina mpango kabisa wa kuingia kwenye siasa. Nawaomba wasanii wanaotaka kuingia kwenye siasa kwa lengo la kupata fedha za haraka, waachane na mipango hiyo kwani wananchi wanahitaji mtu wa kuwasimamia shida zao,” alisema Skyner.
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments