Open top menu
Jumatano, 20 Novemba 2013

TIMU ya Afrika Kusini imefanikiwa kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya mabingwa wa dunia, Hispania katika mchezo wa kirafiki uliochezwa leo usiku nchini Afrika Kusini.

Bao pekee katika mchezo huo lilifungwa na Bernard Parker dakika ya 56 na kufanya mchezo huo kumalizika kwa matokeo hayo na kuwaacha mabingwa hao ambao walikuwa wamekamilika uwanjani kutoambulia kitu.

Katika mchezo mwingine wa kirafiki wa kimataifa uliozikutanisha timu za Ujerumani na England uliochezwa kwenye Uwanja wa Wembley ulimaliza kwa Three Lions kushindwa kulipa kisasi na kukubali kipigo cha bao 1-0.

England na Ujerumani walikutana kwa mara mwisho mwaka 2010 kwenye fainali za Kombe la Dunia na kukubali kipigo cha mabao 4-1 katika hatua ya robo fainali na kuyaaga mashindano hayo.


Bao pekee katika mchezo huo lilifungwa na beki wa Arsenal Per Martesacker katika ya 39 na kufanikiwa kudumu hadi mwisho wa mchezo huo.
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments