Open top menu
Jumanne, 19 Novemba 2013

NI muujiza pekee ndiyo utakaoupeleka timu ya taifa ya Misri katika fainali za Kombe la Dunia Brazil 2014, katika mchezo wao wa marudiano dhidi ya Ghana unaochezwa leo jijini Cairo.

Misri ili wafanikie kutinga katika fainali hizo na kuungana na Ivory Coast, Nigeria na Cameroon wanatakiwa kuifunga Ghana mabao 5-0 kutokana na kukubali kipigo cha mabao 6-1 katika mchezo wa kwanza uliochezwa jijini Kumasi nchini Ghana.

Mshambuliaji wa Ghana, Asamoah Gyan amesema pamoja na kuibuka na ushindi mnono katika mchezo wa kwanza lakini lolote linaweza kutokea katika soka.

Mechi nyingine ambayo inatarajiwa kutoa timu ya tano ya Afrika itakayokwenda nchini Brazil katika fainali hizo, ni kati ya Burkina Faso ambao watakuwa ugenini kuvaana na Algeria.


Mchezo huo ambao unatarajia kuwa na ushindani mkubwa kutokana na mchezo wa kwanza kumalizika kwa Algeria kupoteza mchezo huo kwa kipigo cha mabao 3-2.
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments