Open top menu
Jumatano, 27 Novemba 2013

MABAO mawili ya kiungo Jack Wilshere leo yameipa ushindi wa 2-0 Arsenal dhidi ya Marseille ya Ufaransa katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya usiku huu Uwanja wa Emirates.

Ilimchukua sekunde 29 tangu kuanza kwa mchezo huo kiungo huyowa England kufunga bao la kwanza akimtungua kipa hodari, Steve Mandanda na akfunga tena bao la pili dakika ya 65. 

Nayo Barcelona jana ilionja joto ya jiwe baada ya kukubali kichapo cha mabao 2-1 kutoka kwa Ajex katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya mjini Amsterdam. Pamoja na ushindi huo, Ajax ilimaliza pungufu ya mchezaji mmoja baada ya Veltman kutolewa nje kwa kadi nyekundu dakika ya 48.

Mabao ya Ajax yalifungwa na Serero dakika ya 18 na Hoesen dakika ya 41 kabla ya Xavi kuifungia Barca bao la kufutia machozi kwa penalti dakika ya 49.
 

Katika mchezo mwingine, Chelsea imefungwa bao 1-0 na FC Basle, bao pekee la Mohamed Salah. Mabao ya Kaka dakika ya 12, Zapata dakika ya 49 na Balotelli dakika ya 59 yameipa AC Milan ushindi wa 3-0 dhidi ya Celtic nchini Scotland katika mchezo mwingine wa michuano hiyo. 






Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments