Open top menu
Jumanne, 5 Novemba 2013

LIGI ya Mabingwa Ulaya inatarajia kuendelea tena leo na kesho katika viwanja mbalimbali, lakini leo miamba 16 itashika uwanjani kuwania pointi tatu ili kujiweka vizuri katika nafasi ya kucheza hatua ya mtoano wa michuano hiyo mikubwa barani Ulaya.

Katika michezo hiyo nane lakini mechi ambazo zinatarajia kuteka hisia za mashabiki wa soka duniani kote ni mchezo wa mabingwa watetezi Bayern Munich pamoja na mabingwa wa zamani Real Madrid na Manchester United.

Hapa chini ni michezo hiyo itakavyokuwa kwa kifupi

Real Sociedad v Man Utd
United watajihakikishia kucheza 16 bora kama watapata ushindi Hispania baada ya kushinda mchezo wa kwanza 1-0 nyumbani kwao dhidi ya Sociedad, ambayo inacheza kwa mara ya kwanza michuano hiyo baada ya miaka 10.  Manchester inaongoza kundi hilo kwa pointi saba baada ya mechi tatu.

Sociedad imefunga bao moja katika mechi tatu za Ligi ya Mabingwa hadi sasa na haina pointi yoyote, lakini ushindi wake wa mabao 5-0 iliyopata dhidi ya Osasuna ni ishara njema kabla ya mchezo wa leo.

Shakhtar v Bayer Leverkusen
Timu zote mbili zimefungwa katika ligi za kwao wiki hii, Shakhtar wamenyukwa 2-0 na Volyn Lutsk, kikiwa ni kipigo cha tatu mfululizo kwao, huku Leverkusen wakinyukwa1-0 na timu ya mkiani Eintracht Braunschweig.

Leverkusen ilishinda katika mchezo wa kwanza walipokutana Shakhtar mwezi uliopita, ushindi huo umewafanya kufikisha pointi sita, moja nyuma ya vinara Manchester United.

Juventus v Real Madrid
Real Madrid imekusanya pointi tisa katika michezo mitatu baada ya Cristiano Ronaldo kufunga mabao mawili wakishinda 2-1 dhidi ya Juventus walipokutana mara ya mwisho na sasa wanahitaji sare tu kutoka kwa timu hiyo ya Turin kujihakikishia kufuzu kwa16 bora. 

Copenhagen v Galatasaray
Galatasaray ilishinda mechi ya kwanza kwa mabao 3-1 mjini Istanbul na kupanda hadi nafasi ya pili wakiwa nyuma kwa pointi tano kwa Real, lakini mbili zaidi ya Juve na tatu kwa Copenhagen.

PSG v Anderlecht
Mabingwa wa Ufaransa wamefuzu kwa hatua ya mtoano kwa mwaka wa pili mfululizo baada ya kuichakaza Anderlecht kwa mabao 5-0 katika mchezo uliopita na kuweka rekodi ya kushindi mechi zote tatu katika kundi hilo.

Manchester City v CSKA Moscow
City iliweka kado ubaya wa hali ya hewa na kufanikiwa kuifunga CSKA wiki mbili zilizopita katika mchezo ulioharibika kwa kashfa ya ubaguzi wa rangi. 

Ushindi dhidi ya miamba hiyo ya Russia utawahakikisha kufuzu kwa hatua ya mtoano kwa mara ya kwanza baada ya kushindwa kufanya hivyo mara mbili chini ya Roberto Mancini.

Viktoria Pilsen v Bayern Munich
Mabingwa watetezi wamethibisha kuwa hawafungiki kama PSG, walithibisha hilo Jumamosi waliposhinda 2-1 dhidi ya Hoffenheim na kuweka rekodi ya kutofungwa katikaBundesliga na kuifikia rekodi ya Hamburg iliyoweka kati Januari 1982 na Januari 1983 waliposhinda mechi 36.



Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments