Open top menu
Jumanne, 19 Novemba 2013

TIMU ya Taifa ya Ghana pamoja na kupoteza mchezo wake wa leo usiku dhidi ya Misri kwa mabao 2-1 lakini wamefanikiwa kufuzu kucheza fainali za Kombe la Dunia 2014 za nchini Brazil, katika mchezo uliochezwa jijini Cairo, nchini Misri.

Ghana imefuzu hatua kwa jumla ya mabao 7-3 baada ya kushinda kwa ushindi mnono wa mchezo wa kwanza kwa mabao 6-1 mchezo uliochezwa jijini Kumasi.

Misri ambayo iliingia uwanjani ikiwa na nia ya kupata ushindi wa mabao 5-0 ili waweze kufuzu katika fainali hizo lakini walijikuta hadi wanaenda mapunziko wakiwa mbele kwa bao moja lililofungwa na Amr Zaki dakika ya 24.

Waarabu hao walikuwa na kasi katika kipindi cha pili wakisaka mabao manne lakini walilazimika kusubiri hadi dakika ya 84 ambapo Gedo aliongeza bao la pili kabla ya Kevin-Prince Boateng kuipatia Ghana bao la kufutia machoni katika mchezo huo dakika ya 89.


Ghana inaungana na Ivory Coast, Nigeria na Cameroon ambazo tayari zimeshafuzu hatua hiyo na wanaisubiri mshindi kati ya Burkina Faso na Algeria ambao unachezwa kwa sasa. Katika mchezo wa awali Burkina Faso walishinda mabao 3-2.
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments