Open top menu
Ijumaa, 15 Novemba 2013

KOCHA wa zamani wa Azam, Stewart Hall amesaini mkataba wa kufundisha chuo kipya cha Sunderland cha Kidongo Chekundu kwa lengo la kuibua na kukuza vipaji vya wachezaji nchini.

Akizungumzia jana baada ya kusaini mkataba huo, Hall alisema amefurahi kupata nafasi hii hapa Tanzania katika mpango huu wa kuendeleza vipaji vya wachezaji vijana katika klabu zote  na timu ya taifa.

“Chipukizi watakuwa wakifundishwa mbinu, ufundi, nguvu na kuwaandaa kwa ajili ya kucheza soka ya kisasa.  Pia kutakuwa na mafunzo ya ukocha.”

Hall aliongeza, “Wachezaji watakaokuwa bora zaidi watakuwa wakipata nafasi ya kufanya majaribio katika akademi ya Sunderland ya Light Uingereza.”

Mtendaji Mkuu wa Symbion Power Tanzania, Peter Gathercole alisema Hall atakuwa meneja wa kijiji cha michezo cha Kidongo Chekundu Sports Park na Elite Football Academy.

Gathercole alisema ujenzi wa kituo hicho utakaoanza mwezi huu utakuwa na viwanja vya kisasa 3G vyenye nyasi bandia na viwanja vitano vidogo kulingana na umri.  Pia kutakuwa na vyumba vya kubadilishia nguo, vyumba vya matibabu na sehemu ya chakula.

Naye Mkurugenzi wa Sunderland AFC, Margaret Byrne, alisema: “Tungependa kuona akademi hii inakamilika kwa wakati. Tumemchagua Stewart kuendeleza chuo hiki ni matumaini yetu kila mmoja atajitoa katika kuhakikisha tunapata matunda yake katika siku za karibuni.”

Hall, ambaye ni kocha mwenye leseni ya UEFA na mkufunzi wa UEFA, hivi karibuni alivunja mkataba wake na klabu ya Azam.


Pia, aliwahi kuifundisha timu ya taifa ya Zanzibar, alikuwa Mkurugenzi wa akademi ya Birmingham City.  Mbali na hiyo Hall aliwahi kuwa kocha timu ya taifa ya Saint Vincent na Grenadines na timu ya Pune FC ya India.
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments