Open top menu
Jumapili, 3 Novemba 2013

VIJANA wa Arsene Wenger wanaedhamilia kumaliza kiu ya mataji kwa Arsenal baada ya jana kuendelea kujikita kileleni mwa msimamo wa Ligi Kuu England wakiwa na tofauti na pointi tano na anayemfuata.

Arsenal wamefikia pointi 25 wakiwa kileleni baada ya jana kuitandika Liverpool mabao 2-0 wakifuatiwa na Chelsea wenye pointi 20 katika msimamo huo sawa na Liverpool waliokuwa nafasi ya tatu.

Katika mchezo huo ambao ulikuywa na ushindani mkali lakini Arsenal walionekana kutawala mchezo huo kwa muda mrefu, walipata bao la kwanza kupitia kwa Santi Cazorla dakika ya 19 wakati bao la pili lilifungwa na Aaron Ramsey dakika 59.

Matokeo hayo yanaweza kuwapa nguvu Arsenal ambao wanasafiri kwenda Ujerumani kuvaana na Borussia Dortmund katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya utakaochezwa Jumanne.
Mshambuliaji wa Manchester United, Wayne Rooney akifunga bao la tatu katika mchezo wa jana.

Katika mchezo mwingine wa ligi hiyo, Manchester United wameendelea kufufuka baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Fulham United na kuwafanya kufikisha pointi 17 wakiwa katika nafasi ya nane katika msimamo wa ligi hiyo.

Mabao ya United yamefungwa na Antonio Valencia, Robin van Persie na Wayne Rooney na kuwafanya kuongeza matumaini ya kutetea taji lao la ubingwa wa ligi hiyo.

Manchester City jana walivuna ushindi mnono wa mabao 7-0 dhidi ya Norwich City mchezo uliochezwa kwenye Uwanja wa Etihad jijini Manchester.

Pazia la mabao la City lilifungulia na bao la kujifunga la Bradley Johnson wakati mengine yalifungwa na David Silva, Matija Nastasic Alvaro Negredo, Yaya Toure, Sergio Aguero na Edin Dzeko alikamilisha kalamu ya mabao katika mchezo huo.


Siku ya jana ilikuwa mbaya kwa Chelsea baada ya kukubali kipigo cha mabao 2-0 kutoka kwa Newcastle United, shukrani kwa mabao ya  Yoan Gouffran na Loic Remy. 
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments