Open top menu
Jumamosi, 23 Novemba 2013

BONDIA Mtanzania Omari Kimweri  'Lion Boy' anayefanya shughuli zake Deer Park, Victoria, nchini Australia anatarajia kuwa mtanzania wa kwanza kupanda ulingoni  Novemba 30, mwaka huu  kugombea ubingwa wa Dunia unaotambuliwa na  WBC uzito wa kg 47.5.

Mpambano huo utakaopigwa nchini ya China na bingwa wa dunia wa uzito huo nchini humo, Xiong Zhao Zhong ambaye ndiye anayeshikilia taji hilo la ubingwa wa dunia WBC.

Kimweri anakuwa mtanzania wa kwanza kuwania taji kubwa kabisa duniani akitokea nchini Austalia huku sapoti kubwa akitegemea kutoka Tanzani ambapo alipozaliwa. 

Kigezo cha kufanya apate pambano hilo kubwa ni kutokana na rekodi yake pamoja na kutakiwa bondia mwenye asili ya Afrika ambapo kula imemdondokea Kimweri kwa mara ya kwanza mtanzania huyo ataonekana Dunia nzima akijaribu kuwania ubingwa wa WBC.


Kimweri kwa sasa yupo katika mazoezi ya mwisho ya kujiandaa na mpambano huo amesema kuwa yeye binafsi yupo tayari kabisa kwa mpambano huo, amewaomba Watanzania waendelee kumuombea kwani maombi hayo yatamsaidia kunyakua taji hilo.
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments