Open top menu
Alhamisi, 21 Novemba 2013

KITENDO cha Shirikisho la Mpira wa Miguu la Kimataifa (Fifa) kutangaza kuongeza muda wa kupiga kura za kumchaguza mchezaji bora wa dunia ‘Ballon d’Or 2013 kutoka Novemba 15 hadi Novemba 29 kimekuwa na faida kubwa kwa Cristiano Ronaldo.

Maamuzi hayo yametafsiriwa ni kama ya kumbeba Cristiano Ronaldo dhidi ya wapinzani wake kama Lionel Messi, Franck Ribery na Zlatan Ibrahimovic, baada ya nahodha huyo wa Ureno kupiga hat trick dhidi ya Sweden na kuipa tiketi timu yake ya Taifa kukata tiketi ya fainali za kombe la dunia 2014.


Mwisho wa makocha, manahodha na waandishi wanaopiga kura hizo kuwasilisha majina matatu ya juu ilikuwa November 15, saa kadhaa baada ya kumalizika kwa michezo ya hatua ya mtoano na Rebery anayecheza Bayern Munich alikuwa akipewa nafasi zaidi ya kuibuka na ushindi wa tuzo hiyo.
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments