Open top menu
Alhamisi, 21 Novemba 2013

Na Erasto Stanslaus
SIMBA ya Dar es Salaam imeanza kufuata nyayo za msimu uliopita wa Ligi Kuu ya Bara zilizoifanya ianze vizuri lakini ikaishia kushika nafasi ya tatu.

Klabu hiyo ilianza msimu ikiwa na kocha Milovan Cirkovic lakini katikati ya msimu ikamtimua na nafasi yake ikachukuliwa na Mfaransa, Patrick Liewig aliyetimuliwa mwishoni mwa msimu.

Msimu huu, Simba ilianza kunolewa na Abdallah Kibaden akisaidiwa na Jamhuri Kihwelu ambao wametupiwa virago. Taarifa zinasema kwamba ataajiriwa Zdravko Logarusic wa Croatia aliyewahi kuifundisha Gor Mahia ya Kenya.

Katikati ya msimu uliopita Simba, uliibuka mgogoro wa uongozi ambao ulipelekea baadhi ya wajumbe wa Kamati ya Utendaji kujiuzulu. Msimu huu Kamati ya Utendaji imemsimamisha Mwenyekiti wake, Ismail Aden Rage.

Sababu za kusimamishwa kwake ni danadana kuhusiana na ziliko fedha za uuzwaji wa mchezaji wao Emmanuel Okwi pamoja na kutojishughulisha sana na masuala ya klabu. Okwi aliuzwa katika klabu ya Étoile du Sahel ya Tunisia kwa dola 300 (Sh. 480 milioni).

Rage ndiye alifanya mazungumzo na Étoile na ndiye aliyekamilisha dili la kumuuza lakini fedha hizo hazikufika klabuni. Fedha hizo ndiyo sababu ya kukorofishana na tawi la Mpira Pesa.


MAKALA IMETOKA GAZETI LA MAWIO
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments