Open top menu
Jumatatu, 18 Novemba 2013

KWA mara ya saba timu ya taifa ya kandanda ya Cameroon imefaulu kuingia fainali za kombe la dunia mwaka 2014 nchini Brazil baada ya kuwachapa Tunisia 4-1 mjini Yaounde.

Mwezi uliopita wakati mataifa hayo mawili yalipokutana katika uwanja wa Rades , nchini Tunisia matokeo yalikuwa suluhu ya kutofungana bao lolote.

Lakini katika mechi iliyochezwa mjini Yaounde , siku ya Jumapili jioni mshambuliaji Pierre Webo alifungua mvua ya mabao baada ya safu ya ulinzi ya Tunisia kufanya masihara.

Na kabla ya kwenda mapumzikoni Benjamin Moukandjo aliifungia Cameroon bao la pili kabla ya mchezaji wa akiba Ahmed Akaichi kuipatia Tunisia bao lao moja na la pekee muda mfupi baadae.

Lakini kabla ya firimbi ya mwisho mchezaji Jean Makoun aliiongezea Cameroon mabao mawili ya chap chap na kufanya matokeo kuwa 4-1 hivyo kuipa Cameroon tiketi ya kuwa timu mojawapo zitakazo wakilisha Afrika katika kombe la dunia nchini Brazil mwaka 2014.


Awali ,timu za Ivory Coast na Nigeria zilikuwa tayari zimejikatia tiketi ya kuwa wawakilishi wengine wa Afrika katika mashindano hayo ya mwaka 2014.
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments