Open top menu
Jumanne, 19 Novemba 2013

BAADA ya wanachama wa Simba kuhaha kutaka kumng’oa madarakani Mwenyekiti wao, Ismail Aden Rage sasa dua zao zimetimia baada ya Kamati ya Utendaji ya klabu hiyo kumsimamisha.

Kikao hicho kilichofanyika jana jijini Dar es Salaam kilifikia maamuzi hayo kutokana na madai ya kuwa kiongozi huyo wa juu wa Simba kukiuka miiko ya uongozi na kukiuka katiba ya klabu hiyo.

Hatua hiyo inakuja siku moja baada ya Rage kuwasainisha mkataba wachezaji wawili kutoka Zanzibar Ally Badru na Awadh Juma aliyekuwa anacheza Mtibwa.

Mabosi wa Simba wamethibitisha kusimamishwa kwa Rage na muda huu wanazungumza na waandishi wa habari sababu za kuchukua maamuzi hayo magumu.

Taarifa ya awali inadai kuwa Rage amekuwa hajishughulishi kwa karibu na timu hiyo lakini pia amekuwa akikiiuka baadhi ya mambo ndani ya katiba na ndio maana kamati ya utendaji imepata nguvu ya kumsimamisha kwenye kikao hicho cha jana.


Baadaye tutakuletea taarifa za kina zaidi juu ya maamuzi hayo
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments