Open top menu
Alhamisi, 7 Novemba 2013

KOCHA Mkuu wa klabu ya Azam FC, Stewart John Hall ameitosa kwa mara nyingine timu hiyo muda mchache baada ya kumalizika kwa mchezo wao dhidi ya Mbeya City ambao uliomalizika kwa sare ya mabao 3-3.

Kocha huyo raia wa Uingereza mara baada ya kumalizika kwa mchezo huo aliwaaga wachezaji wake pamoja na benchi la ufundi baada ya kukubaliana na uongozi wa klabu hiyo.

Hall kuiacha Azam ni mara ya pili kwani mara ya kwanza aliondoka katika kikosi hicho Agosti mwaka jana lakini alirudi tena baada ya timu hiyo kumtaka kocha huyo alejee tena kuinoa klabu hiyo.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na klabu hiyo kupitia tovuti yake, imedai kuwa wameachana na Hall ambaye ameomba kufanya hivyo kwani anataka kupata changamoto mpya kutoka katika klabu nyingine.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa pande zote mbili zimekubalina kuvunja mkataba huo baada ya mazungumzo marefu na uongozi unamtakia kila la kheri huko aendako na unamshukuru kwa mafanikio aliyoipatia timu hiyo.

Hall anaiacha Azam ikiwa katika nafasi ya pili katika msimamo wa ligi hiyo baada kujikusanyia pointi 27 huku ikiwa na rekodi ya kutopoteza mchezo katika mzunguko wa kwanza.

Muingereza huyo aliondoka baada ya kuiwezesha Azam kushika nafasi ya pili katika Ligi Kuu na Kombe la Kagame, pamoja na kuiwezesha kutwaa Kombe la Mapinduzi na nafasi yake ikachukuliwa na Mserbia, Boris Bunjak.

Hata hivyo, baada ya mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu msimu uliopita, Stewart aliyehamia Sofapaka ya Kenya, alirejeshwa Azam kufuatia kutimuliwa kwa Mserbia, Bunjak.

Stewart akarudia kuipa nafasi ya pili Azam katika Ligi Kuu na kuipa Kombe la Mapinduzi pamoja na kuiwezesha kutwaa taji la Ngao ya Hisani, michuano iliyofanyika mjini Kinshasa, DRC, Desemba mwaka jana.

Bado haijajulikana sasa Azam itaangukia mikononi mwa kocha gani, ikiwa sasa mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu umemalizika na wachezaji wanakwenda mapumzikoni.


Stewart ni kocha wanne kuondolewa Azam tangu ianze kucheza Ligi Kuu msimu wa 2007/2008 baada ya Wabrazil Neider dos Santos na Itamar Amorin na Mserbia Bunjak.
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments