Open top menu
Jumatano, 20 Novemba 2013

MSHAMBULIAJI wa Ureno, Cristiano Ronaldo ameipeleka timu yake katika fainali za Kombe la Dunia nchini Brazil 2014 baada kufunga mabao matatu ‘hat trick’ katika ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Sweden.

Mchezo huo ambao uliwakutanisha mastaa wawili ambao ni manahodha wa timu hizo, Ronaldo anayeichezea Real Madrid na Zlatan Ibrahimovic anayekipiga katika timu ya PSG ya Ufaransa wote walikuwa wanawania nafasi ya kucheza fainali hizo pamoja na timu zao.

Ronaldo ambaye ndiye mfungaji wa bao la pekee katika mchezo wa kwanza uliochezwa wiki iliyopita nchini Ureno, alifunga bao la kwanza dakika ya 50 kabla ya Ibrahimovic kusawazisha dakika ya 68.

Ibrahimovic aliongeza bao la pili dakika ya 72 lakini dakika tano baadaye Ronaldo alimaliza matumaini ya Sweden kucheza fainali hizo mwakani baada ya kufua bao la pili. 

Wakati Sweden wakisaka bao la kuongoza ili wafufue matumaini ya kucheza fainali hizo, Ronaldo alizima kabisa ndoto hizo baada ya kupachika bao la tatu dakika ya 79 na kufanya mchezo huo umalizike kwa jumla ya mabao 4-2.

Nayo ufaransa imefanikiwa kutinga katika fainali hiyo baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 katika mchezo wake dhidi ya Ukraine shukrani mabao ya Mamadou Sakho dakika ya 22, Karim Benzema dakika ya 34 na bao la kujifunga na Oleg Gusev dakika ya 72. 


Timu nyingine zilizofanikiwa kutinga katika fainali hizo ni Ugiriki ambayo ilitoka sare na Romania ya mabao 1-1 lakini imefuzu kwa jumla ya mabao 4-2, wakati Croatia nayo wamepenya katika hatua hiyo baada ya kuifumua Iceland mabao 2-0.
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments