Open top menu
Jumatatu, 11 Novemba 2013

NYASI za uwanja wa shule ya msingi Ubungo jijini Dar es Salaam leo zinatarajiwa kuwaka moto wakati timu ya wanamuziki wa bendi ya Extra Bongo na kundi la Sanaa ya Maigizo la Jakaya watakaposhuka dimbani kumenyana katika mechi ya kirafiki maalumu kwa ajili ya kuzindua 'Extra Bongo Funs'.

Kwa mujibu wa msemaji wa bendi hiyo Juma Kasesa, maandalizi ya mchezo huo yamekamilika ambapo kwa wiki kadhaa sasa vikosi vya timu zote vimekuwa kwenye mazoezi makali kujiwinda na mchezo unaovuta hisia za mashabiki wa soka waliokamia kumuona Mkurugenzi wa Extra Bongo Kamarade Ally Choki akicheza beki wa kati (mkoba).

Alisema, mechi hiyo ni muendelezo wa bendi hiyo kuongeza wigo mpana wa marafiki kwa ajili ya kujiimarisha katika ushindani wa muziki wa dansi lengo lengo likiwa ni kuwafikia popote walipo.

Alieleza, mchezo huo licha ya kudumisha urafiki wao pia utasaidia kuimarisha afya ya miili ya wachezaji wa pande zote mbili ili kukabiliana na magonjwa nyemelezi na mara baada ya mechi hiyo wameshaomba kukipiga na kundi lingine la sanaa Bongo Movie.

Aliwataja baadhi ya nyota wa bendi hiyo watakaoshuka dimbani wakiongozwa na nahodha wao Salum Chakuku 'Chakuku Tumba' kuwa ni Athanas Muntanabe, Super Nyamwela, Redo Mauzo, Efraim Joshua, Adam Hassan, Hosea besi, Danger Boy, Adam Bombole na Ally Koncho ambao wameapa kuadhibu wapinzani kutokana tambo nyingi ambazo wamekuwa wakizitoa dhidi yao.

Kwa upande Mkurugenzi wa Jakaya Arts linalorusha mchezo wake katika kituo cha runinga cha ITV kila Jumamosi, Devid Mponji, alisema, wamejiandaa vya kutosha kuikabili Extra Bongo na kwa kiwango cha safu yake ya ushambuliaji Choki atakuwa uchochoro wa kuruhusu kufungwa mabao mepesi kwakuwa hatoweza kumudu kasi waliyonayo.


Alisema,kikosi chake kinanolewa na kocha wa timu ya Kijogoo maarufu kwa jina 'Kikoti'  chini ya nyota wake Erick Mikongoti, Rashidi Mawala, Omary Zero na nahodha Jose Mawala.
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments