Open top menu
Alhamisi, 7 Novemba 2013

Mshambuliaji wa Yanga, Jerry Tegete akifunga bao la pili katika mchezo wao dhidi ya JKT Oljoro

HESABU zilizokuwa zikipigwa na wachezaji, viongozi, benchi la ufundi na mashabiki wa Yanga, zimetimia na kufanikiwa kuongoza Ligi Kuu Tanzania Bara katika mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo.

Yanga walikuwa wakihitaji ushindi katika mchezo wao dhidi ya Oljoro huku ikitaka mchezo kati ya Mbeya City na Azam uliochezwa Chamanzi umalizuike kwa sare na hayo ndiyo yaliyotokea katika mchezo huo.

Mabao matatu yaliyofungwa na Simon Msuva dakika ya 23 na Mrisho Ngassa dakika ya 30 na lile la tatu lililofungwa na Jerry Tegete yalitosha kuifanya Yanga imalize mzunguko wa kwanza ikiwa kileleni baada ya kutimiza pointi 28 baada ya kucheza michezo 13. 

Katika mchezo wa Chamanzi Azam walilazimishwa sare na Mbeya City ya mabao 3-3 na kuifungulia njia Yanga kukaa kileleni baada ya kuwazidi kwa pointi mbili.

Azam na Mbeya City ambao walikuwa kileleni kwa pointi 26 na sare hiyo timu zote sasa zimefikiwa pointi 27 huku Azam wakiwa nafasi ya pili wakati Mbeya itakuwa nafasi ya tatu kwa tofauti na mabao ya kufunga na kufungwa.


Nafasi ya nne katika msimamo wa ligi hiyo inashikiliwa na Simba wenye pointi 24 baada ya kushinda mchezo wake wa jana dhidi ya Ashanti United.
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments