Open top menu
Jumatatu, 11 Novemba 2013

WAAMUZI watatu wa Tanzania wameteuliwa na Baraza la Vyama vya Mpira wa Miguu Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) kuwa miongoni mwa waamuzi 18 watakaochezesha michuano hiyo huku Watanzania wakiwa wawili tu.

Michuano ya Cecafa mwaka huu imepangwa kuanza kutimua vumbi kuanzia Novemba 27 mwaka huu jijini Nairobi, Kenya, Tanzania itawakilishwa na waamuzi, Israel Mujuni mwamuzi wa kati na Fedinard Chacha mwamuzi msaidizi wakati Waziri Sheha kutoka Zanzibar ni mwamuzi wa kati.

Katibu Mkuu wa Cecafa, Nicholas Musonye alisema waamuzi hao waliotangazwa wamegawanyika katika makundi mawili, nane ni waamuzi wa kati wakati nane ni waamuzi wasaidizi.

Musonye alisema waamuzi hao wanatakiwa kufika Nairobi kabla ya kuanza kwa michuano hiyo huku wakiwa wamejiandaa kwa kupimwa afya zao pamoja na kuwa fiti.

Waamuzi wa kati waliokuwa katika orodha hiyo na nchi zao kwenye mabano ni Anthony Okwayo (Kenya), Denis Batte (Uganda), Wish Yabarow (Somalia), Louis Hakizimana (Rwanda), Thiery Nkurunziza (Burundi), Gebremichael Luleseged (Eritrea) na Kheirala Murtaz (Sudan).

Waamuzi wasaidizi ni Gilbert Cheruiyot (Kenya), Tonny Kidiya (Kenya), Mark Sonko (Uganda), Suleiman Bashir (Somalia), Fraser Zakara (Sudan Kusini), Simba Honore (Rwanda), Hamid Idam (Sudan) na Kinfe Yimla (Ethiopia).


Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments