Open top menu
Ijumaa, 8 Novemba 2013

ALIYEKUWA golikipa namba moja wa Simba na timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars, Juma Kaseja amesema anasubiri kupewa fedha walizokubaliana na Yanga ili asaini kuichezea klabu hiyo.

Kaseja amesema tayari amefanya mazungumzo na klabu hiyo ya Yanga ambayo aliwahi kuitumikia kwa msimu mmoja 2008/2009 kabla ya kurejea Simba msimu uliofuata na kuipa ubingwa wa rekodi ya bila kufungwa hata mchezo mmoja wakipata sare mbili chini ya kocha raia wa Zambia Patrick Phiri.

Kipa huyo ambaye alimaliza mkataba na Simba na klabu hiyo kukataa kumuongeza mkataba mwingine amesema wamekubaliana na Yanga kila alichohitaji na anachosubiri ni klabu hiyo kumpatia fedha walizokubaliana ili asaini mkataba.

"Bado sijasaini Yanga lakini kweli nimefanya nao mazungumzo na makubaliano yote tumeafikiana lakini nitasaini baada ya kupewa fedha tuliyokubaliana,wakinipa fedha hata leo nasaini"alisema Kaseja. 

Kipa huyo maarufu kwa uhodari wake langoni anasema mpira ndio kazi yake kwahiyo anaweza kucheza kwenye klabu yoyote inayomuhitaji na kufikia naye makubaliano na ndio maana hata Yanga walipomfuata amekaa nao na kufikia makubaliano yanayosubiri kutia saini mkataba.

Akiwa Yanga msimu wa 2008/2009 Kaseja aliandika rekodi ya kuwa kipa aliyefunga goli katika mchezo wa ligi kuu, akitumbukia wavuni kwenye mchezo uliopigwa kwenye uwanja wa CCM Kirumba Yanga walipocheza dhidi ya Toto Africans ambao kwasasa wapo ligi daraja la kwanza.


Baada ya kumaliza mkataba wake na Simba Juni mwaka huu klabu ya FC Lupopo ya Congo DRC ilijaribu kumsajili lakini mpango huo ukashindwa kukamilika baada ya kutokea matatizo kadhaa ikiwemo kukamatwa kwa wakala aliyekuwa akishughulikia mpango huo huku mkataba nao ukiwa umetumwa kwa lugha ya kifaransa.
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments