Open top menu
Jumanne, 19 Novemba 2013

MCHEZO wa leo kati ya Sweden na Ureno ndiyo utakaoamua ni staa gani kati ya Cristiano Ronaldo na Zlatan Ibrahimovic ataenda kwenye fainali za Kombe la Dunia za 2014 zitakazofanyika nchini Brazil.

Mchezo huo wa marudio utachezwa kwenye Uwanja wa Solna jijini Solna nchini Sweden ambapo katika mchezo wa kwanza Sweden walikiubaki kichapo cha bao 1-0 liulilofungwa na Ronaldo katika mechi iliyochezwa jijini Instabul nchini Ureno.

Katika mchezo huo Sweden wanahitaji ushindi wa mabao 2-0 ili waweze kusonga mbele katika michuano hiyo na mshambuliaji na nahodha wake, Ibrahimovic atakapoa nafasi nya kushiriki fainali hizo.

Kocha wa Ureno, Paolo Bento ametamba kuibuka na ushidni katika mchezo huo na amewatahadharisha wapinzani wake kuwa kama watakuwa makini kumzuia Ronaldo basi wachezaji wengine watafunga tu na kuwapaleka Brazil.

Bento ambaye anauhakika na kuibuka na ushindi katika mchezo huo baada ya kushinda mechi ya kwanza na kuweza kumdhidhitibi nahodha wa Sweden, Ibrahimovici.

Michezo mingine ya kuwania kufuzu fainali hizo itakayochezwa leo Ufaransa watakuwa na kibarua kigumu watakaporudiana na Ukraine mechi itakayopigwa kwenye Uwanja wa Saint Denis.

Katika mchezo huo Ufaransa inahitaji ushindi ili waweze kufuzu kucheza fainali hizo za mwakani, timu hiyo ipo katika hali mbaya kutokana na kupoteza mchezo wao wa kwanza kwa kipigo cha mabao 2-0.  


Mechi nyingine ni Romania watakuwa nyumbani kuwakaribisha Ugiriki kwenye Uwanja wa Bucharest, Croatia       watakuwa wenyeji wa Iceland kwenye dimba la Zagreb.
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments