Open top menu
Jumanne, 19 Novemba 2013

TIMU ya taifa ya Algeria leo usiku imekata tiketi ya kucheza Kombe la Dunia nchini Brazil 2014 na kuwa timu pekee ya kiarabu kutoka Afrika itakayoshiriki michuano hiyo mwakani.

Algeria wamefanikiwa kufuza kucheza fainali hizo baada leo usiku kuiondosha Burkina Faso katika mbio hizo baada ya kushinda mchezo kwao bao 1-0 na kufanya matokeo ya jumla kuwa mabao 3-3, hivyo wao kupenya na faida ya mabao ya ugenini. Mchezo wa awali Burkina Faso walishinda mabao 3-2.

Waarabu hao wametinga hatua hiyo na kuwaacha wenzao Misri iliyoondolewa na Ghana wakati Tunisia walitupwa na Nigeria katika hatua ya makundi.

Shujaa wa Algeria katika mchezo huo alikuwa Madjid Bougherra aliyeifungia timu yake bao pekee katika mchezo huo na kuikatia tiketi ya Brazil timu yake katika dakika ya 49.
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments