Open top menu
Jumanne, 5 Novemba 2013

MZUNGUKO wa kwanza wa Ligi Kuu Tanzania Bara unatarajia kumalizika kwa michezo ya kesho Novemba 6 na keshokutwa Novemba 7 huku kukiwa na sintofahamu nani atamaliza akiwa kileleni.

Imekuwa na mazoea kuwa katika ligi hiyo timu zinazokuwa kileleni ni Yanga, Azam na Simba SC lakini msimu huu ni tofauti kutokana na ushindani ulioibuka kutoka kwa timu kama Mbeya City.

Mbeya City, timu ambayo ni mpya katika ligi hiyo imeongeza ushindani mkubwa na kuna uwezekano ikamaliza mzunguko wa kwanza ikiwa katika kileleni mwa msimamo. 

Timu hiyo inayonolewa na Juma Mwambusi ipo katika nafasi ya pili katika msimamo wa ligi hiyo ikiwa na pointi 26 sawa na vinara Azam FC na timu hizo zitamaliza mzunguko huo kwa kuvaana mechi ambayo itatoa maamuzi nani atakuwa kinara.

Michezo ya mwisho itakuwa kama ifuatavyo, Novemba 6 ni JKT Ruvu na Coastal Union Uwanja wa Chamazi, Ashanti United na Simba Uwanja wa Taifa, Kagera Sugar na Mgambo Shooting Uwanja wa Kaitaba, Bukoba na Ruvu Shooting dhidi ya Mtibwa Sugar Uwanja wa Mabatini.

Novemba 7 kutakuwa na mechi kati ya Azam FC na Mbeya City Chamazi, Yanga itacheza na Oljoro JKT kwenye Uwanja wa Taifa, wakati Rhino itakuwa mwenyeji wa Tanzania Prisons Uwanja wa Ally Hassan Mwinyi Tabora.

Mechi ambazo zinatarajiwa kuteka hisia za mashabiki wa soka nchini ni zitakazochezwa Novemba 7 kati ya Yanga na Oljoro, lakini kwa maana ya mechi ya kufungia msimu, basi itakuwa Chamazi Azam na Mbeya City.

Mshindi wa mechi hiyo moja kwa moja atamaliza mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu akiwa kileleni, na atakayefungwa anaweza kuporomoka hadi nafasi ya tatu, iwapo Yanga SC itashinda mechi yake na Ojoro. Wakitoka sare, Azam itabaki juu ya Mbeya City na Yanga inaweza kupanda kileleni ikishinda.

Mbeya City na Azam ndizo timu pekee ambazo hadi sasa msimu huu hazijapoteza mechi, wakati mabingwa watetezi, Yanga waliopoteza mechi moja tu mbele ya Azam, wanakaa nafasi ya tatu kwa pointi zao 25.



Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments