Droo ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya ‘Uefa’
imepangwa hivi karibuni na timu za Barcelona na Arsenal ndiyo timu ambazo
zimepangwa kwenye makundi magumu kuliko miamba mingine ya soka barani Ulaya.
Katika droo hiyo Barcelona wamepangwa kundi H pamoja
na AC Milan ya Italia, Ajax Amsterdam ya Uholanzi na Celtic ya Scotland ambapo
katika kundi hilo timu mbili ndizo zinakazosonga mbele katika hatua ya 16 bora.
Kwa upande wa Arsenal na wenyewe watakuwa na kibarua
kigumu katika hatua ya makundi ambapo wapo kwenye F wakiwa na Olympique
Marseille ya Ufaransa, Borussia Dortmund ya Ujerumani na Napoli ya Italia.
Michezo ya msimu wa 59 ya michuano hiyo mikubwa
barani Ulaya hatua ya makundi inatarajia kuanza Septemba 17, 2013 wakati
fainali za michuano hiyo zinatarajiwa kupigwa kwenye Uwanja wa da Luz uliopo jijini
Lisbon, Ureno Mei 24, 2014.
MAKUNDI
YA UEFA
Kundi A:
Manchester United, Shakthar, Leverkusen, Real
Sociedad
Kundi B:
Real Madrid, Juventus, Galatasaray, FC Copenhagen
Kundi C:
Benfica, PSG, Olympiacos, Anderlecht
Kundi D:
Bayern Munich, CSKA Moscow, Man City, Viktoria Plzen
Kundi E:
Chelsea, Schalke, FC Basel, Steaua Bucuresti
Kundi F:
Arsenal, Marseille, Dortmund, Napoli
Kundi G:
FC Porto, Atletico Madrid, Zenit, Austria Vienna
Kundi H:
Barcelona, AC Milan, Ajax, Celtic
0 comments