Open top menu
Jumanne, 20 Agosti 2013



ULIMWENGU wa soka una kiu ya kuona jinsi ya wachezaji nyota duniani, Lionel Messi na Neymar watakapocheza pamoja katika kikosi cha FC Barcelona msimu huu. Lakini pamoja na kuwepo kwa hamu hiyo pia wachezaji hao kila mmoja atakuwa na cha kujifunza kitu kutoka kwa mwenzake.

Kwa kuwa Messi ni mchezaji bora wa dunia kwa sasa, kuna uwezekano mkubwa wa Neymar kujifunza vitu vingi kutoka kwa nyota huyo kuhusu soka na maisha kwa ujumla.

Angalia mambo saba ambayo Neymar atajifunza kutoka kwa Messi na akiyafuata vizuri ni wazi kuwa Mbrazil huyo atakuja kuwa tegemeo katika siku za usoni.

Jinsi ya kudanganya
Messi na Neymar tayari wana vitu ambavyo vinafanana vya kufanyiwa sana faulo na mabeki, lakini Messi ana uwezo mkubwa wa kutumia ujanja wake kuwahadaa mabeki ili wamuangushe na kupata faulo ambazo mara nyingi zinafaida kwa timu yake, Neymar ambaye silaha yake kubwa ni kujiangusha anatakiwa kusoma ujanja huo wa Messi ambaye hutumia zaidi mguu wake wa kulia kwa kuuacha nyuma na mabeki hujikwaa na kumuangusha.

Uvumilivu
Kutokana na uchanga wake katika soka, Neymar anatakiwa kusoma somo la uvumilivu kutoka kwa Messi. Neymar anapokuwa na mpira huwa na haraka ya kutaka kwenda mbele ili kufunga lakini kwa Messi huamini kwa kupiga pasi huku wakitawala mpira na mwisho wake hupata goli ambalo hulitafuta kwa mipango.

Umuhimu wa kujituma
Wachezaji wa Barcelona huwa wanajituma kwa lengo la kusaka ushindi na wanapoona mambo ynakuwa magumu hurudisha mpira nyuma kwa Messi na kuanza mashambulizi upya kwa kuwa wanaamini kuwa anaweza kuumiliki mpira, Neymar hana sifa hiyo ya kurudi nyuma na kuanza upya akifika eneo la hatari, hicho anatakiwa kujifunza kwa Messi.

Kutengeneza bao na kufunga vina muhimu sawa
Wachezaji hawa wawili wote ni mafundi kwa kuzifumania nyavu duniani. Lakini unaweza kuwa mchezaji bora zaidi bila ya kufunga mabao. Messi ana uwezo mkubwa wa kuwaunganisha wachezaji kwa kuwatengenezea nafasi za kufunga kitu ambacho kimekosekana kwa Neymar na ili awe mchezaji bora anatakiwa kujifunza hicho kwa Messi.

Uwiano wa majivuno na unyenyekevu
Ili uwe mchezaji bora duniani unatakiwa kuwa na uwiano wa majivuno na  unyenyekevu, Neymar ukiacha kupata mafanikio akiwa bado mchezaji mchanga lakini pia ndiyo umri wake pia unakua, mtu sahihi wa kumwambia hiki hapana na hiki kizuri ni Messi kwa kuwa amepitia katika hatua hizo.

Ushirikiano
Hili ni somo kubwa sana kwa Neymar kulisoma kutoka kwa Messi kwani mshambuliaji huyo kwake mafanikio ya klabu ndiyo kitu muhimu kuliko yake binafsi. Neymar anatakiwa kuiga mfano wa Messi kwa kuisaidia kwanza Barcelona na mafanikio yake yatakuwa baadaye.

Jinsi gani atakuwa bora
Kuna tofauti ya kuwa mshindi na kuwa mfalme. Messi ni mmoja kati ya washindi katika soka kwa sasa, ameshinda tuzo nne ya uchezaji bora duniani. Neymar ni mchezaji chipukizi mwenye mafanikio kwa sasa, anatakiwa kujifunza kwa Messi anawezaje kuwa bora zaidi ya alivyosasa.
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments