William, muda mfupi baada ya kutua London asubuhi ya leo kwa ajili ya vipimo tayari kukipiga Spurs
KLABU ya Tottenham iko karibu kumsajili kiungo wa kimataifa wa Brazil, Willian, baada ya mchezaji huyo kuonekana katika Jiji la London mchana huu kwa ajili ya vipimo vya afya.
Kiungo huyo mwenye miaka 25 yuko karibu zaidi kujiunga na Spurs, kwa uhamisho ambao unakadiriwa kufikia pauni milioni 30.
Liverpool ilikuwa klabu inayodhaniwa ndiyo iliyokuwa karibu kumsajili mchezaji huyo, ambapo ilikuwa ikimfuatilia kwa ukaribu nyota huyo wa timu ya Anzhi, ambapo pia alikuwa akitakiwa na Arsenal, lakini amesafiri hadi London asubuhi ya leo kwa ajili ya kupimwa afya na klabu ya Spurs leo.
0 comments