Open top menu
Alhamisi, 22 Agosti 2013


Mwanamuziki mkongwe wa muziki wa dansi nchini, Muhidin Maalim 'Gurumo'


MWANAMUZIKI mkongwe wa kundi la Msondo Ngoma, Muhidin Mwalimu 'Gurumo', ametangaza rasmi kustaafu shughuli za muziki.

Akizungumza Dar es Salaam jana, Gurumo, alisema ameamua kustaafu muziki kwa sababu ya umri wake kuwa mkubwa na kushindwa kumiliki vizuri changamoto za kazi hiyo.

Gurumo alisema amekuja kuwaaga rasmi mashabiki wake kuwa muziki hataki kuendelea nao tena na ameona apumzike na kuendelea na majukumu ya kulea familia yake vizuri.

"Tangu nimeanza muziki 1954 hadi sasa sijapata hata baiskeli katika kazi yangu hii, hivyo nimeona suala la msingi ni kuuacha nikiwa na umri huu.

"Licha ya kustaafu muziki, sitawatenga wasanii pamoja na kundi langu, nitaendea kuwa pamoja nao na nitaendelea kuwa mshauri wao pale nitakapohitajika kufanya hivyo," alisema Gurumo.

Aliongeza kuwa ameteuwa kamati kwa ajili ya kumsaidia mambo yake mengine ikiwa ni pamoja na harakati za kuwaaga mashabiki wake kisanii.

''Tumeanda tamasha kwa kushirikiana na kamati niliyoiteua, ambalo nitapanda jukwani kuimba kwa mara ya mwisho na kuwaaga kama nilivyoingia," aliongeza.

Nguli huyo aliwaasa wasanii wa nchini kuimba muziki wenye kujenga kama zamani na si kukimbilia kuimba Bongo Flava, kwani muziki huo ni wa kisasa, huku akimtaja Diamond kuwa ndiyo mwanamuziki anayempenda zaidi katika muziki wa kizazi kipya.
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments