Open top menu
Jumatatu, 26 Agosti 2013

Deco de Souza





KIUNGO wa zamani wa timu za Barcelona na Chelsea, Deco, ametangaza rasmi kustaafu soka siku ya sherehe yake ya kuzaliwa kutimiza miaka 36 mwaka huu.


Nyota huyo wa kimataifa wa Ureno alianza soka yake katika klabu ya Salgueiros nchini Brazil kabla ya kuhamia Porto 1999, na kuwa raia wa nchi hiyo.


Kutokana na ushiriki wa klabu hiyo katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya 2004, aliondoka na kuhamia Primeira Liga akiichezea Barcelona, akitumia miaka kwa miamba hiyo ya Camp Nou kabla ya kutua Stamford Bridge kwa misimu miwili.


Aliondoka katika soka ya Ulaya akiwa bado na kiwango kizuri 2010, na alirudi Brazil kwenda kuitumikia klabu ya Fluminense, na kuamua kutundika daluga baada ya miaka mitatu akiwa na miamba hiyo ya Amerika Kusini.


"Kwa majonzi na masikitiko makubwa, natangaza kuwa huu ndiyo mwisho wa kucheza soka ya kimataifa," alinukuliwa akisema hivyo katika mtandao wa AS.


"Dakika ya mwisho nikiwa na Fluminense Jumatano iliyopita ilikuwa ya mwisho katika uchezaji wa soka yangu ya kimataifa kwa miaka 17 sasa.


"Ningependa kuendelea hadi mwisho wa Ligi Kuu ya hapa (Brasileiro) na kuifanya timu yangu kurudi katika michuano ya Libertadores, lakini mwili wangu hauwezi kuniruhusu.


"Nina furaha sana kwa kufikia mafanikio haya na uaminifu wa mashabiki katika timu zote nilizowahi kuzitumikia."


Kiungo huyo mshambuliaji aliitumikia Ureno kwa michezo 75 ndani ya miaka saba aliyopanza kuitumikia timu hiyo ya taifa, akiiwakilisha timu katika michuano mikubwa miwili ya Kombe la Ulaya na miwili ya Kombe la Dunia.
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments