Ofisa Habari wa TFF, Boniface Wambura
TIKETI
za elektroniki zitaanza kutumika katika mzunguko wa nne wa Ligi Kuu ya Vodacom
(VPL) utakaoanza Septemba 18 mwaka huu. Tayari benki ya CRDB ambayo ndiyo
ilishinda tenda hiyo imeshakamilisha ufungaji wa vifaa kwa ajili ya matumizi ya
tiketi hizo katika viwanja vyote.
Hivi
sasa Serikali ambayo ndiyo inamiliki Uwanja wa Taifa, Shirikisho la Mpira wa
Miguu Tanzania (TFF) pamoja na CRDB zinashughulikia mfumo wa tiketi hizo kwenye
uwanja huo ambao ndiyo ulikuwa haujakamilika kwa matumizi katika upande huo.
Kwa
mujibu wa Ofisa Habari wa TFF, Boniface Wambura, mfumo (system) ulioko kwenye
uwanja huo inapishana na ule utakaotumiwa na CRDB, hivyo pande husika
zinashughulikia suala hilo ili mifumo hiyo iweze kuingilia.
0 comments