Nyota ya bondia wa Tanzania, Francis Cheka imezidi
kung’ara baada ya kumtwanga kwa pointi bondia kutoka Marekani, Phill Williams
katika mpambano wa raundi 12 wa kuwania mkanda wa dundia wa Shirikisho la Ngumi
za Kulipwa Duniani (WBO).
Cheka ambaye alionekana kutawala mpambano huo toka
raundi ya kwanza alifalifanikiwa kumwangusha mpinzani wake lakini aliendelea na
kumaliza hadi raundi ya mwisho.
Bondia huyo ambaye hana mpinzani hapa nchini
amekabidhiwa mkanda wake WBO.
0 comments