Kiungo wa Bayern, Bastian Schweinsteiger
KIUNGO wa timu ya soka ya Bayern Munich, Bastian
Schweinsteiger, anaweza kuukosa mchezo wa fainali ya Uefa Super Cup dhidi ya Chelsea
baada ya kuumia kifundo cha mguu katika mechi ya sare ya bao 1-1 dhidi ya Freiburg.
Schweinsteiger alilazimika kutolewa baada ya kucheza
kwa dakika 10 wakati Bayern ikianza kwa kuongoza kwa bao lililofungwa Xherdan
Shaqiri.
Lakini Freiburg walichomoa Nicolas Hofler dakika ya 88
na kukiacha kikosi cha kocha Pep Guardiola kukosa nafasi ya kujiongezea ponti
tatu muhimu huku ikimkosa Schweinsteiger.
" Schweinsteiger ameumia kifundo cha mguu (ankle),”
kocha huyo Mhispania alisema. “Atafanyiwa vipimo kesh. Nafikiri anaweza kucheza
Ijumaa, lakini bado hatulijui hilo.
"Tulicheza vizuri. Lakini ukiwa unaongoza kwa
1-0 katika ligi ya Bundesliga, vitu kama hivi vinaweza kutokea. Hatukuacha
kushambyulia na tulikuwa na nafasi kadhaa. Lakini najivunia sana kuwa na wachezaji
kama hawa.”
Nahodha wa Bayern, Philipp Lahm alikubaliana na
maoni ya kocha wake, akiamini kuwa yeye na wenzake wanapaswa kujilaumu wenyewe
kwa kupata sare hiyo.
“Tujilaumu wenyewe,” Lahm aliuambia mtandao wa klabu
yake (fcbayern.telekom.de). “Tuliruhusu bao la kusawazisha kabla ya mchezo
kumalizika, lakini tulikuwa na nafasi ya kuongeza mabao zaidi kabla hata ya
kusawazisha kwao.
“Kama tungekuwa na mabao zaidi isingekuwa hivi.
Katika mechi chache zilizopita, tumeshindwa kupata matokeo kwa tatizo kama hili,
na huwa tunaadhibiwa kwa hilo.”
0 comments