Open top menu
Ijumaa, 30 Agosti 2013


Mshambuliaji Robin van Persie leo ametangazwa kuwa mchezaji bora wa timu hiyo kwa mwezi wa Agosti wa Manchester United, ikiwa ni tuzo yake ya kwanza tangu alipotua katika klabu hiyo akitokea Arsenal.

Straika huyo wa kimataifa wa Uholanzi amefanikiwa kutawazwa kuwa mchezaji bora wa mwezi baada ya kupata 57% ya kura zilizopigwa wakati Nemanja Vidic alipata 26% na aliyeshika nafasi ya tatu ni Danny Welbeck alipata 17%.

Van Persie ambaye ameichezea Manchester United michezo 50 ya mashindano yaote tangu atue klabuni hapo, ametwaa tuzo hiyo baada ya kufanikiwa kufunga mabao manne katika michezo mitatu aliyocheza mwezi huu.

“Siku zote kushinda tuzo ni jambo zuri sana, hasa unapopigiwa kura na mashabiki,” alisema Vana Persie.
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments