Shindano la Big Brother Africa msimu wa nane
lililopewa jina la ‘The Chase’ limefikia kikomo leo na ni zamu ya Dillish.
Dillish raia wa Namibia ndiye aliyeibuka kidedea
katika shindano hilo na kufanikiwa kubeba kitita cha dola 300,000. Mwanadada
huyo alifanikiwa kubwaga washiriki wengine walioingia kwenye hatua ya tano
bora.
Walioingia kwenye tano bora mbali ya Dillish ni Beverly,
Melvin, Cleo na Elikem. Wa kwanza kutoa katika hatua hiyo alikuwa Beverly,
akafuatiwa na Melvin kabla ya Elikem naye kuwafuata wenzake na wakabakia wawili
Cleo na Dillish.
Pamoja na mchuano kuwa mkali kwa wawili hao lakini
nyota ilimwangukia Mnamibia huyo na kutawazwa kuwa mshindi wa nane wa shindano
hilo.
0 comments