Kikosi cha Fenerbahce
TIMU ya soka ya Fenerbahce imefungiwa kwa miaka
miwili kushiriki katika mashindano ya Ulaya na Mahakam ya Usuluhishi ya masuala
ya michezo ya kimataifa (CAS).
Tamko hilo limetolewa muda si mrefu nchini Uturuki,
ambapo limetokana na kesi yao ya msingi ya kudaiwa kupanga matokeo katika
michuano ya Ulaya msimu uliopita.
Miamba hiyo ya Uturuki ilichapwa jumla ya mabao 5-1
na Arsenal katika michuano ya awali kufuzu kwa michuano ya Ligi ya Mabingwa
Ulaya, ambapo ilifungwa 3-1 nchini kwao kabla ya jana kukubali kichapo cha
mabao 2-0.
0 comments