Open top menu
Jumatano, 28 Agosti 2013


Kocha wa PSV Eindhoven, Phillip Cocu 




KOCHA wa timu ya soka ya PSV Eindhoven, Phillip Cocu, amesema timu yake imejiandaa kwa lolote wakati timu yake ikijiandaa kuivaa AC Milan kwa ajili ya mchezo wa marudianbo wa kufuzu kwa Ligi ya Mabingwa Ulaya.

PSV na Milan wanakutana katika Uwanja wa San Siro leo baada ya kwenda sare ya bao 1-1 Jumatano iliyopita, ambapo miamba hiyo ya Uholanzi ililazimika kusawazisha bao waliloruhusu mapema kwenye mchezo huo.

Na wakati miamba hiyo ya Italia ikihitaji hata suluhu kuweza kufuzu na kuingia katika hatua ya makundi, Cocu ana uhakika kuwa timu yake inaweza kuibuka na ushindi wa ugenini.

“Kucheza nyumbani ni tofauti na unapokuwa ugenini,” alianza kwa kusema Cocu. “Tulicheza mchezo mzuri tulipokuwa Eindhoven na nina uhakika kuwa tutacheza vizuri pia leo katika mchezo wetu wa mjini Milan.

“Ni wakati mzuri kwangu na pamoja na timu kwa ujumla, nah ii inakuja pale ambapo tunaona tunaweza kushindana na timu ngumu kama Milan.

“Hii inaleta wasiwasi mkubwa wakati mwingine, lakini ni wasiwasi chanya, ni kitu ambacho unahitaji kuwanacho katika soka. Kazi yangu pia ni kusaidia wachezaji kupata uzoefu huu na kukabiliana na presha.

“Tumejiandaa kwa kila kitu. Sijui Milan watakuja na mbinu gani, kama watazuia ama watashambulia. Kwa mchezo kama huu muhimu, chochote kinaweza kutokea katika makosa madogo.”

Milan itakuwa ikimkaribisha tena kiungo wa kimataifa wa Brazil, Robinho na beki kinda, Mattia De Sciglio, baada ya wachezaji hao kuwa fiti kwa ajili ya mchezo huo.

Hata hivyo, Cocu bado hana matumaini licha ya Milan kufungwa mabao 2-1 dhidi ya Hellas Verona katika mchezo wa Ligi Kuu ya Italia ‘Serie A.

“Milan ina uwezo mkubwa wa kuchagua aina ya wachezaji wazuri wa kuwatumia,” Cocu alisema. “Tunatakiwa kuingia uwanjani tukijua kabisa kuwa tuna wajibu wa kuwazuia wachezaji hawa.”
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments