Klabu ya Chelsea imemgeukia mshambuliaji wa Anzhi
Makhachkala, Samuel Eto’o baada ya kushindwa kumng’oa straika wa Manchester
United, Wayne Rooney ambaye klabu yake imegoma kumuuza kwa mahasimu wao hao.
Klabu hiyo yenye maskani yake jijini London ipo
katika mazungumzo na mwakilishi wa mchezaji huyo ambaye tayari amekubali
makubaliano ya awali ambnapo Chelsea nimepanga kumpa mkataba wa miaka miwili.
Eto'o tayari ameonyesha nia ya kuhamia Chelsea lakini
dili hilo linapata nguvu zaidi baada ya Jose Mourinho ambaye tayari ana
washambuliaji wanne lakini hadi sasa hakuna aliyeifungia bao timu hiyo,
washambuliaji hao ni Fernando Torres, Romelu Lukaku na Demba Ba.
Mshambuliaji huyo wa zamani wa kimataifa mwenye
miaka 32, anatarajiwa kusaini mkataba katika klabu hiyo kwa ada ya uhamisho ya
paundi 1.7 milioni. Mpango huo unaweza kukamilika kwa haraka kutokana na klabu
ya Anzhi Makhachkala kupunguza gharama kwa mchezaji huyo.
0 comments