Open top menu
Jumapili, 25 Agosti 2013


Msanii Judith Wambura ‘Lady Jaydee akipagawisha kwenye tamasha la Kili Music Tour lililofanyika kwenye Ukumbi wa Mbeya City Mjini Mbeya.

TAMASHA la wasanii la Kili Music Tour juzi (Jumamosi) llifanyika kwenye Ukumbi wa New Mbeya City Club, ambapo wasanii mbalimbali walitoa burudani ya aina yake.

Katika tamasha hilo ambalo limedhaminiwa na Kampuni ya Bia Tanzania kwa kupitia bia yake ya Kilimanjaro, wasanii mbalimbali wa muziki wa kizazi kipya na Hip Hop walitoa burudani kali na kuwaacha mashabiki midomo wazi kutokana na kufanya kile ambacho hawakutegemea.

Katika tamasha hilo, ambalo lilihudhuriwa na maelfu ya mashabiki wa muziki kutoka katika Mkoa wa Mbeya na maeneo ya karibu, lilianza jioni ambapo msanii mwenyeji Awilo wa Mbeya alianza kwa kuimba baadhi ya nyimbo ikiwa ni pamoja na zile za asili.

Baada ya msanii huyo, alipanda jukwaani Snura na kuimba baadhi ya vibao vyake ikiwa ni pamoja na Nimevurugwa na Majanga ambavyo viliwafanya mashabiki walipuke kwa kumshangilia kwa kiasi kikubwa.

Baadaye alipanda Linex ambaye alionekana kukonga nyoyo za mashabiki wake kutokana na staili tofauti aliyoingilia na kushuka chini ya jukwaa ambapo aliimba sambamba na mashabiki wake.

Barnaba Elius alipanda baada ya kushuka kwa Linex, na kuimba baadhi ya nyimbo na baadaye alifuatia Ben Paul na kuimba nyimbo kadhaa ikiwa ni pamoja na wimbo wake mpya wa Wa Ubani aliomshirikisha Alice.

Kwenye tamasha hilo ambalo limebeba ujumbe wa Kikwetu kwetu,  lilimfanya Kala Jeremiah aliyejizolea tuzo nyingi za Kilimanjaro Music Awards, kuamsha hisia za watu kutokana na kuimba nyimbo kama vile Dear God, Ningekuwa Rais na Wimbo wa Taifa.

Izzo Business ambaye ndio alikuwa msanii mwenyeji kwenye tamasha hilo aliwafanya mashabiki wake wamshangilie kwa staili ya tofauti kutokana na kuimba nyimbo kama vile Ongea na Mshua, Nakuchukia Mwaka jana na Love Me aliyemshirikisha Barnaba Elius.

Wasanii wa Hip Hop Farid Kubanda ‘Fid Q’ na Joseph Haule waliwafanya mashabiki kuwa na hisia kali kutokana na tng zao kiasi ya kwamba Polisi waliokuwa wakiangalia usalama kufanya kazi ya ziada na kuwalazimisha kushuka jukwaani kabla ya kupanda kwa Judith Wambura ‘Lady Jaydee na baadaye Profesa Jay alipomalizia onyesho hilo kwa kuimba baadhi ya nyimbo ikiwa ni pamoja na zile za zamani kama vile Niamini, Piga Makofi, Hapo Vipi na Kamili Gado.
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments